Sunday, September 2, 2012

UJUE UISLAAMU HALISI

Assalaam Alaykum,baada ya kuyajua hayo tuliyoyajua kuhusiana na NINI UISLAAM NA NANI NI MUISLAAM,NA NANI SI MUISLAAM.Leo tuendelee na kipengele kingine cha maana ya neno DINI.UISLAAM huliangalia neno Dini kwa maana iliyotofauti na waichukuliayo Wasiokuwa Waislaam!Wasiokuwa Waislaam hulichukulia neno Dini kwa maana ya Imani juu ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.Kwa mfano katika Katika Kamusi ya Kiingereza ya A.S Horbi with A.B Lowide,A.C Gimson,Oxford Advanced Leaner's Dictionary of current English,Oxford University Press,Nairobi(1962) Ukurasa wa 713,neno Religion(Dini) limefasiriwa hivi "Beliefin the existence of Supernatural ruling power,the Creator and Controller of the universe,Who has given to Man a Spiritual nature which continues to exist after the death of the body"
Tafsiri yake ni kuwa "Dini ni Imani ya kuwepo Mungu Muumba,aliye Muweza na Mwenye Nguvu juu ya kila kitu.Mmiliki wa Ulimwengu ambaye amempa Binaadamu Roho ambayo huendelea kuishi baada ya kifo cha mwili"
Aidha katika Kamusi ya Kiswahili Sanifu neno Dini limetafsiriwa kama ifuatavyo "Imani inayohusiana na Mambo ya kiroho baina ya Binaadamu na Mwenyezi Mungu,au njia ya kuhusiana na Mwenyezi Mungu".Kwa tafsiri hizi Makafiri wao hudai kuwa hawana Dini kwa kuwa hawana Imani juu ya kuwepo kwa Mwenyezi Mungu.
Lenin mmoja wa wasomi wa Kikafiri anasema "Every body must be absolutely free to profess any Religion he pleases or no Religion whatever,i.e to be a Atheist which every socialist is as a rule...." Tafsiri yake ni kuwa "Kila Mtu hana budi kuwa huru kabisa kufuata Dini yoyote anayoitaka au asiwe na Dini kabisa,yaani awe Kafiri,jambo ambalo inambidi kila mjamaa awe hivyo...."
Neno Dini katika Lugha ya Kiarabu hufasiriwa kama Mila,Utamaduni,Desturi,Njia,Utratibu au Mfumo fulani.Katika Uislaam Neno Dini maana yake ni "Utaratibu au Mfumo wa Maisha ulioanzishwa na Mwenyezi Mungu au Kiumbe".Kwa maana hiyo hakuna Mtu asiyekuwa na Dini kwani ni lazima Mtu awe amefuata utaratibu fulani ambao aidha amejipangia mwenyewe au amepangiwa!
Na kwa mtazamo wa Uislaam Dini(Mifumo ya Maisha) ipo mingi tu,ndio maana Mtume aliambiwa aseme kuwaambia Makafiri kuwa "NYINYI MNA DINI YENU,NA MIMI NINA DINI YANGU"(Sura ya 106 Aya ya 6).Kwa maana nyingine Mtume alikuwa akiwaambia kuwa "NYINYI MNA MFUMO WENU WA MAISHA,NA MIMI NINA MFUMO WANGU WA MAISHA"Tofauti ni kuwa Mfumo aliokuwa akiufuata Mtume umetungwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe na Mfumo waliokuwa wakiufuata Makafiri walijitungia wenyewe!
"INNAD DIINA INDALLAAHIL ISLAAM..."Mwenyezi Mungu ananadi kupitia kinywa cha Mtume(s.a.w),yenye Tafsiri kwamba "HAKIKA DINI INAYOKUBALIKA MBELE YA MWENYEZI MUNGU NI UISLAAM"(Sura ya 3 Aya ya 19).Ukiyakunjua zaidi maneno hayo kwa maana ya neno Uislaam na neno Dini tulizokwishaziona ni kuwa "HAKIKA MFUMO WA MAISHA UNAOKUBALIKA MBELE YA MWENYEZI MUNGU NI WAKUTII NA KUNYENYEKEA AMRI,SHERIA NA HUKUMU ZA MWENYEZI MUNGU"
Na kwa kumalizia somo letu kwa Siku ya leo,namalizia kwamba "NA ANAYETAFUTA DINI ISIYOKUWA YA UISLAAM,HAITOKUBALIWA KWAKE.NAYE AKHERA ATAKUWA NI MIONGONI MWA WENYE HASARA"(Sura ya 3 Aya ya 85).Nayo tukiikunjua inakuwa "NA ANAYETAFUTA MFUMO WA MAISHA USIOKUWA WA KUTII NA KUNYENYEKEA AMRI,SHERIA NA HUKUMU ZA MWENYEZI MUNGU,HAUTOKUBALIWA KWAKE.NAYE AKHERA ATAKUWA NI MIONGONI MWA WENYE HASARA"
Shime ndugu zangu tuishi katika Utaratibu na Mfumo aliouridhia Allah!
"SOMO LITAENDELEA INSHAALLAH......."

No comments:

Post a Comment