Sunday, September 2, 2012

SOMO LA MUENDELEZO WA MADHEHEBU

Assalaam Alaykum, Kumbukeni kuwa huu ni Uwanja mpana  unaruhusiwa kutoa maoni yako kwa namna ulivyojaaliwa ili mradi usimtukane Mtu wala kumdhalilisha!Ndugu zangu tutumie Akili na Fikra zetu,laa sivyo tutaenda kuhukumiwa kwa hilo!ALLAH anasema "NA KWA HAKIKA TUTAWAINGIZA JAHANNAM WENGI KATIKA MAJINI NA WATU.WANA MIOYO LAKINI HAWAFAHAMII KWAYO,NA WANA MACHO LAKINI HAWAONI KWAYO,NA WANA MASIKIO
LAKINI HAWASIKII KWAYO.HAO NI KAMA WANYAMA BALI WAO WAMEPOTEA ZAIDI.HAO NDIO WALIOGHAFILIKA"(Sura ya 7 Aya ya 179).
Akasema tena kuwa "HIKI (QUR'AN) NI KITABU TULICHOKITEREMSHA KWAKO ILI ZIZINGATIWE AYA ZAKE NA ILI WAKUMBUKE WENYE AKILI"(Sura ya 38 Aya ya 29).Na namalizia kwa kauli yake kuwa "......NA(MWENYEZI MUNGU) HUJAALIA UCHAFU KWA WALE WASIOTUMIA AKILI"(Sura ya 10 Aya ya 100).Aya zote hizo zinaonesha umuhimu wa utumiaji wa Akili na Fikra zetu katika kuyaendea mambo ya msingi,kwani ndicho kitu kinachomtofautisha Mwanaadamu na Wanyama wengine!Haiwezekani wakati wa Usiku Mtu akwambie kuwa huu ni Mchana nawe ukubaliane nae pasi na kufikiri!
Lakini vilevile,nilitoa Dondoo za udadisi ambazo zingemsaidia Mchangiaji katika kutoa maoni yake!Kwamba ikiwa Muongozo umekemea vikali juu ya Madhehebu(Makundi) na kuiorodhesha kuwa ni Ukafiri na Ushirikina,na ikiwa Mtume(s.a.w) hakuacha hali ya Umakundi(Madhehebu) ndani ya Uislaam!Je nini kilichosababisha hali hii ya umakundi ndani ya Uislaam?
Dodoso lingine likasema,Je hali hii ya Umakundi(Madhehebu) ndani ya Uislaam inaweza kuondoka na Dini kurudi kama wakati wa Enzi za Mtume(s.a.w)?
Somo litaendelea inshaallah....!

No comments:

Post a Comment