Sunday, September 2, 2012

MUENDELEZO WA SOMO LA MADHEHEBU

Assalaam Alaykum!Naam tuendelee na kufahamishana mawili matatu kuhusiana Uislaam!Baada ya kuona makemeo ya Allah juu ya kuigawanya Dini na kuwa Makundi Makundi(Madhehebu) kwa kutuonesha kuwa kufanya hivyo ni Ukafiri na ni Ushirikina!Tuone basi ni kipi hicho CHANZO CHA MADHEHEBU KATIKA UISLAAM!Jambo ambalo ndio Mada ya Siku yetu ya leo!
Ndugu zangu,Njama za kuugawa Uislaam hazikuanza jana wala juzi,bali tangia Enzi za Bwana Mtume Muhammad(s.a.w).Jambo hilo la kuigawa Dini lilikuwa likifanyika kila mara anapoletwa Nabii/Mtume wa Mwenyezi Mungu kwa lengo la wale wenye kutawala waendelee kuwatawala Watu ambao wakishaujua Ukweli kuhusiana na Maisha yao kwa ujumla hawatokuwa na njia nyingine ya kuwatawala.
Jambo hilo ililazimu wale wanaotaka kuendelea kutawala,wapambane na Manabii wa Mwenyezi Mungu kwa kuiviza na kuifahamisha vingine ile Haki iliyokwisha kuja kwa lengo lao hilo.Sitaki tuzame sana huko lisije Somo letu likawa refu sana hata Msomaji akashindwa kuzingatia!Turudi sasa katika kuangalia hizo njama zilizokuwa zikifanyika wakati wa Uhai wa Mtume(s.a.w) ili kuwagawa Watu!
Kitu cha Mwanzo walichofanya ni kuwaelekeza Watu na kuwapa mafunzo kinyume cha yale aliyokuwa akifundisha yeye Mtume,na hayo yalifanywa na wale Wanafiki waliokuwa wakijifanya kuwa ni Wanafunzi watiifu wa Mtume hali ya kuwa ni waongo!Hayo Mtume hakuwa akiyajua mpaka alipozinduliwa na Mwenyezi Mungu mwenyewe! "NA WANASEMA TUMETII,NA WANAPOTOKA KWAKO KUNDI MOJA MIONGONI MWAO HUPANGA NJAMA USIKU KINYUME CHA YALE UNAYOYASEMA..." (Sura ya 4 Aya ya 81).
Hawa walikuwa pamoja na Mtume!Wanasikiliza Aya za Mwenyezi Mungu mbele ya Mtume(s.a.w) mwenyewe kisha kumbe wanakuwa hawajaridhika na yale waliyofundishwa na Mtume,na kuamua kukaa vikao vya mapinduzi usiku kupindua yale alowafundisha Mtume!
Wafanya mapinduzi wa kabla ya Mtume walikuwa wakiyaingilia moja kwa moja yale Mafundisho ya Kitabu husika na kuyachakachua!ndivyo ilivyofanywa Taurati,Zaburi na Injili!lakini wafanya mapinduzi hawa wa zama za Mtume Muhammad(s.a.w) walikumbana na mkwamo,pale walipokumbana na Ahadi ya Mwenyezi Mungu kwamba "HAKIKA SISI NDIO TULIOUTEREMSHA UKUMBUSHO(QUR'AN) NA HAKIKA SISI NDIO TUTAKAOULINDA"(Sura ya 15 Aya ya 9)
Kwahiyo zoezi la kutia mafundisho yao ndani ya Kitabu cha Mwenyezi Mungu ili wapate kuwagawa Watu na kuendelea kuwatawala,likagonga mwamba!hata hivyo hawakukata tamaa,wakaona ni bora wamvae Mtume mwenyewe "NA WANAPOSOMEWA AYA ZETU ZILIZO WAZIWAZI,WALE WASIOTARAJI KUKUTANA NASI HUSEMA:LETE QUR'AN ISIYOKUWA HII AU IBADILISHE!SEMA:HAINIFALII MIMI KUIBADILISHA KWA ITAKAVYO NAFSI YANGU.MIMI SIFUATI ILA NINAYOFUNULIWA. HAKIKA MIMI NAOGOPA IKIWA NITAMUASI MOLA WANGU,ADHABU ILIYO KUU"(Sura ya 10 Aya ya 15).
kwa hiyo Jaribio lingine likakwama!Ndio ikawabidi sasa waingie kazini wenyewe kila Mtume anapofundisha hivi wao hutunga mengine ili kuwadanganya Watu na kuwatoa kwenye mstari ili waendeleze mambo yao waliyokuwa nayo kabla ya Mtume Muhammad kupewa Utume!Mwenyezi Mungu anatupa habari kwamba hali hiyo ya kumbadilishia maneno illikuwa ikimhuzunisha sana Mtume,hali iliyomlazimu Mwenyezi Mungu amtulize Mtume wake kwa kumwambia "EWE MTUME!WASIKUHUZUNISHE WALE WAFANYAO HARAKA KUKUFURU,MIONGONI MWA WANAOSEMA KWA VINYWA VYAO:TUMEAMINI NA HALI NYOYO ZAO HAZIJAAMINI,NA MIONGONI MWA MAYAHUDI,WANAOKUSIKILIZA ILI WAKASEME UWONGO,WANAOKUSIKILIZA KWA AJILI YA WATU WENGINE WASIOKUFIKIA.HUBADILISHA MANENO KUTOKA MAUDHUI YAKE..."(Sura ya 5 Aya ya 41)
Hiyo ndio kazi waliokuwa wakiifanya baadhi ya Wanafiki miongoni mwa Maswahaba wa Mtume wakishirikiana na Mayahudi,kutunga Maneno tofauti na alivyofundisha Mtume mwenyewe kama alivyoteremshiwa na Mola wake!Je Maswahaba hawa wazusi tutawajuaje hali ya kuwa Mtume Mwenyewe hakuwa akiwajua!"NA KATIKA MABEDUI WALIO PEMBEZONI MWENU KUNA WANAAFIKI,NA KATIKA WENYEJI WA MADINA PIA KUNA WALIOBOBEA KATIKA UNAAFIKI,WEWE HUWAJUI.SISI TUNAWAJUA.TUTAWAADHIBU MARA MBILI KISHA WATARUDISHWA KATIKA ADHABU KUBWA"(Sura ya 9 Aya ya 101).
Alaa kumbe miongoni mwa Maswahaba wa Mtume walikuwa ni Wanaafiki!halafu mbaya zaidi hata Mtume mwenyewe hakuwa akiwafahamu kwa Majina yao!Je sisi tutawajuaje toba Yaa Rabbi!
Mwenyezi Mungu alimtajia Mtume na Waislaam kwa ujumla,Sifa za wale Maswahaba wanafiki waliokuwa wakishirikiana na Makafiri ili kuwagawa Waislaam na wawe makundi makundi ili Ukafiri uendelee kutawala Duniani.Moja ya Sifa zao ni hii "LAU WANGELITOKA NANYI WASINGELIKUZIDISHIENI ILA MACHAFUKO,NA WANGELIKWENDA HUKU NA HUKO KATI YENU ILI KUKUTILIENI FITNA,NA MIONGONI MWENU WAPO WANAOWASIKILIZA SANA.NA MWENYEZI MUNGU ANAWAJUA MADHALIMU.TANGU ZAMANI WALITAKA KUKUTILIENI FITNA,NA WAKAKUPINDULIA MAMBO CHINI JUU,MPAKA IKAJA HAKI NA IKADHIHIRIKA AMRI YA MWENYEZI MUNGU NA HALI WAMECHUKIA"(Sura ya 9 Aya ya 47-48).Naam,ukianzia Aya za nyuma yake utaona namna Wanaafiki hao walivyokuwa wakihimizwa kwenda kuipigania Dini ya Mwenyezi Mungu nao wakijitia uzito kwenda,lakini kumbe ilikuwa kheri vilevile kwani hawana ambalo wangefanya huko Vitani ila kuitia chokochoko na fitna na kuna hatari ya kuwa wangegawa makundi kwa wengi wao walikuwa wakiwasikiliza sana wao wanaafiki kuliko Mtume!Na tayari walishampindulia mambo chini juu!Kwa kuingiza Mafundisho yao ya uwongo na kusema kuwa Mtume ndiye aliyesema hayo ili kufanikisha mambo yao!kivipi?
"NA WAPO BAADHI YAO WANAOPINDUA NDIMI ZAO KUKISINGIZIA KITABU ILI MDHANIE KUWA HAYO YANATOKA KWENYE KITABU,NA WALA HAYATOKI KATIKA KITABU.NA HUSEMA HAYA YAMETOKA KWA MWENYEZI MUNGU NA HALI HAYATOKI KWA MWENYEZI MUNGU,NA WANAMSINGIZIA MWENYEZI MUNGU UWONGO NA HALI WANAJUA!"(Sura ya 3 Aya ya 78)
Ndugu zangu,kumbukeni kuwa mambo hayo yalikuwa yanafanywa hali ya kuwa Mtume mwenyewe yu hai!Sikwambii alipokuja kufa!Yaani Watu wanatunga mafundisho ya uwongo ili yadhaniwe kuwa nayo ni Mafundisho ya Mwenyezi Mungu kwa lengo la kuwagawa Waislaam!kivipi?Kwa kutunga Mafundisho juu ya jambo moja kwa namna tofauti!Utaambiwa kwamba Mtume Muhammad(s.a.w) alifanya hivi au alitenda hivi!Fundisho ambalo litakuwa tofauti na fundisho lingine ambalo nalo atakuwa amesema au kutenda tofauti!ambalo nalo litatofautiana na lingine tena,katika tukio moja!au kikao kimoja!au mazingira mamoja!na cha ajabu hayo yote yanaweza kuwa kinyume kabisa na Kitabu kilivyoagiza!
Je ni vipi Mafundisho hayo yakaja kuwagawa Waislaam baada ya Mtume kufariki na kuwa katika hali tuionaya hivi sasa!TOA CHOCHOTE UNACHOKIFAHAMU,NA SOMO LITAENDELEA INSHAALLAH!......

No comments:

Post a Comment