Sunday, September 2, 2012

MADHEHEBU KATIKA UISLAAM NI USHIRIKINA NA NI UKAFIRI!


Assalaam Alaykum nyote!ndugu zangu hebu leo tuzungumze kuhusu hili!natanguliza kuomba radhi kwa lugha ngumu ntakayotumia,si kwa nia mbaya bali ni katika namna ya ufikishaji kwani tukiendelea kupambapambana kinafiki tutakuwa hatufiki!Sote tunafahamu kuwa Mgonjwa kama kupona kwake tiba yake ni kuchomwa sindano,japo ataumia ni lazima achomwe ili kupata uzima wake kama kweli tunampenda!
Madhehebu ni wingi wa neno Dhehebu ambalo maana yake ni Kundi la jamii ya watu wenye kufuata mwenendo na mrengo wa namna fulani iliyotofauti na wengine.
Uislaam ni Dini yenye Mfumo maalum ulioelekezwa na Muumba mwenyewe,Mfumo ambao alimpa Mtume wetu Muhammad(s.a.w) ili naye awafundishe watu.Sote tunafahamu kuwa Mtume(s.a.w) mpaka anafariki Dunia hakuacha ndani ya Uislaam Makundi(Madhehebu) katika jamii ya Waislaam.Mtume na wote waliomfuata walikuwa na mwendo wa namna moja,na wote waliokuwa wakiingia katika Uislaam aliokuwa akiuhuisha Mtume(s.a.w) walilazimika kushika mwendo uleule aliokuwa akiufundisha Mtume,NI UPI HUO?
Ni UMOJA wa kila Jambo katika Dini!Mwenyezi Mungu ni Mmoja(ALLAH),Mtume wetu ni Mmoja(Muhammad),Kitabu chetu ni kimoja(Qur'an),Dini yetu ni moja(uislaam).
Mtume(s.a.w) aliwaambia Waislaam "ENYI MLIOAMINI MUOGOPENI MWENYEZI MUNGU UKWELI WA KUMUOGOPA,WALA MSIFE ISIPOKUWA NI WAISLAAM.NA SHIKAMANENI PAMOJA KATIKA DINI YA MWENYEZI MUNGU NA WALA MSIGAWANYIKE!NA KUMBUKENI NEEMA ZA MWENYEZI MUNGU JUU YENU,PINDI MLIPOKUWA MAADUI BASI AKAZIUNGANISHA NYOYO ZENU NA MKAWA NDUGU KWA NEEMA YAKE(QUR'AN).NA MLIKUWA KATIKA UKINGO WA SHIMO LA MOTO BASI AKAKUOKOENI NALO.NAMNA HIVYO MWENYEZI MUNGU ANAKUBAINISHIENI AYA ZAKE ILI MPATE KUONGOKA!"(Qur'an 3:102-103)
Kwa hiyo Mtume alikuwa akilingania Umoja baina ya Waislaam wenye utaratibu mmoja,ambapo Mwenyezi Mungu alimtaka Mtume awakumbushe Historia yao waliokuwa Waislaam kuwa wamekuwa wamoja,ndugu badala ya hali ya utengano na uadui waliokuwa nao kabla ya kuwa Waislaam.Kwahiyo Uislaam ulikuwa ni mmoja,kundi moja-Kundi la Mwenyezi Mungu(Qur'an 58:22) na ni marufuku kuanzisha kundi ndani ya kundi moja la Uislaam!Bali kulikuwa na kundi lingine ambalo ni kundi la Shetani ambalo lilikuwa ni dhidi ya Waislaam.
Mara fulani kule Madina Wanafiki walijaribu kuanzisha Msikiti na wakamuomba Mtume aende kuuzindua.Mtume(s.a.w) kwa kuwa hakuwa akijua Ghaibu(Siri) aliwakubalia,lakini Allah mjuzi wa Ghaibu alimkataza Mtume wake asiende kuuzindua Msikiti huo kwa kuwa waanzilishi wake hawakuwa na lengo zuri katika kuuanzisha Msikiti huo "NA WALE WALIOTENGENEZA MSIKITI KWA AJILI YA KULETA MADHARA NA UPINZANI NA KUWAGAWA WAUMINI,NA KUWA SEHEMU YA KUJIFICHIA YA WALE WALIOMPIGA VITA MWENYEZI MUNGU NA MTUME WAKE ZAMANI......"(Qur'an 9:107).
Ndio kusema kuwa hao walikuwa ni wanafiki ambao Mwenyezi Mungu aliwaumbua!Kumbe miongoni mwa malengo yao ni kuwagawa Waumini!wasiwe kitu kimoja kwa manufaa yao binafsi kinyume na agizo la Mwenyezi Mungu la kuwataka Waislaam wawe ni kitu kimoja,kundi moja lisilo na mpasuko wala mgawanyiko!Mtume akaambiwa "USISIMAME KAMWE NDANI YA MSIKITI HUO..."(9:108)
Ndugu zangu njama za kuwagawa Waislaam zilendelea na kufanyiwa juhudi kubwa tangu enzi za Uhai wa Bwana Mtume Muhammad(s.a.w).Mtume aliwaasa Waislaam kwa kuwaambia hali akiwaonya "WALA MSIWE KAMA WALE WALIOGAWANYIKA NA KUTOFAUTIANA,BAADA YA KUFIKIWA NA UBAINIFU.NA HAO NDIO WATAKAOPATA ADHABU KUBWA KABISA"(Qur'an 3:105).Kumbe tulishonywa kuwa "Wala tusiwe kama wale!"Ina maana walikuwepo watu walikuwa wameigawa Dini yao na wakatofautiana ndani yake!NI KINA NANI HAO?
Hao si wengine bali ni wale waliopewa Uislaam zamani kisha wakauharibu kwa kuugawa makundi makundi na kila kundi likawa linajiona liko sawa.Wana wa Israel walipewa Uislaam kwenye Taurati kupitia Nabii Musa(a.s),wakaugawa Uislaam wao na ukawa Uyahudi,ambao nao uligawika katika makundi(Madhehebu) ya Uzayuni,Uothordox,Usquirs n.k.
Baadae wakapewa Injili kupitia Nabii Isa(a.s),wakauharibu Uislaam wao na waukaufanya kuwa ni Ukristo,ambao nao uligawika katika makundi(Madhehebu) ya Roman Catholic,Lutheran,Anglican n.k.
Sasa Waislaam walitakiwa wasiwe kama hao,wakati huo wao walikuwa ni kundi moja!wakaonywa tena "NYENYEKEENI KWAKE NA MUMUOGOPE NA SIMAMISHENI SWALA,WALA MSIWE MIONGONI MWA WASHIRIKINA.AMBAO WAMEIGAWA DINI YAO NA WAKAWA MAKUNDI MAKUNDI,KILA KUNDI LINAFURAHIA WALIYONAYO"(30:31-32).
Tunapata hitimisho kuwa kumbe Uyahudi na Ukristo ni Ushirikina kwa kuigawa Dini Makundi Makundi(Madhehebu).Tena Allah akaonya kwa mara nyingine kuwa "NA HAWATOKUWA RADHI NAWE MAYAHUDI NA WAKRISTO MPAKA UFUATE MILA YAO.SEMA HAKIKA MUONGOZO WA MWENYEZI MUNGU NDIO MUONGOZO HASWA,NA KAMA UTAFUATA MATAMANIO YAO BAADA ELIMU ILIYOKUFIKIA,HUTAPATA KUTOKA KWA MWENYEZI MUNGU MLINZI WALA MSAIDIZI"(2:120).
Msiba ulioje Waislaam wamefuata yale waliyokatazwa!Baada ya miaka kadhaa kupita tangu Mtume kufariki,Waislaam wakagawika Makundi Makundi(Madhehebu)!Mpaka leo hii Waislaam waliopewa Uislaam katika Qur'an kupitia Mtume Muhammad(s.a.w) wameugawa Uislaam wao na umekuwa ni Usunni,Ushia,Uanswaar Sunna,Uahmadiyya n.k. na katika hayo makundi kuna makundi mengine madogo madogo ndani yake!
Sasa kuhusiana na mambo kama hayo Mtume aliambiwa na mapema kwamba "HAKIKA WALE WALIYOIGAWA DINI YAO NA WAKAWA MAKUNDI MAKUNDI HUNA UHUSIANO NAO WOWOTE,BILA SHAKA JAMBO LAO HILO LIPO KWA MWENYEZI MUNGU,KISHA ATAWAAMBIA YALE WALIYOKUWA WAKIYATENDA"(6:159).
SOMO LITAENDELEA.....
Lakini kwa sasa,Hebu tujadili kwa pamoja,Ni kitu gani kilichowasababisha Waislaam kuwa na Makundi wakati muongozo wao umekemea waziwazi tena kwa maonyo makali ya Ushirikina na Ukafiri?.Na je,Waislaam wanaweza kurudi katika Uislaam mmoja kama
alouacha Mtume(s.a.w)?

No comments:

Post a Comment