MADHEHEBU KATIKA UISLAAM NI USHIRIKINA NA NI UKAFIRI!
Assalaam Alaykum nyote!ndugu zangu hebu leo tuzungumze kuhusu
hili!natanguliza kuomba radhi kwa lugha ngumu ntakayotumia,si kwa nia
mbaya bali ni katika namna ya ufikishaji kwani tukiendelea
kupambapambana kinafiki tutakuwa hatufiki!Sote tunafahamu kuwa Mgonjwa
kama kupona kwake tiba yake ni kuchomwa sindano,japo ataumia ni lazima
achomwe ili kupata uzima wake kama kweli tunampenda!
Madhehebu ni
wingi wa neno Dhehebu ambalo maana yake ni Kundi la jamii ya watu wenye
kufuata mwenendo na mrengo wa namna fulani iliyotofauti na wengine.
Uislaam ni Dini yenye Mfumo maalum ulioelekezwa na Muumba mwenyewe,Mfumo
ambao alimpa Mtume wetu Muhammad(s.a.w) ili naye awafundishe watu.Sote
tunafahamu kuwa Mtume(s.a.w) mpaka anafariki Dunia hakuacha ndani ya
Uislaam Makundi(Madhehebu) katika jamii ya Waislaam.Mtume na wote
waliomfuata walikuwa na mwendo wa namna moja,na wote waliokuwa wakiingia
katika Uislaam aliokuwa akiuhuisha Mtume(s.a.w) walilazimika kushika
mwendo uleule aliokuwa akiufundisha Mtume,NI UPI HUO?
Ni UMOJA wa
kila Jambo katika Dini!Mwenyezi Mungu ni Mmoja(ALLAH),Mtume wetu ni
Mmoja(Muhammad),Kitabu chetu ni kimoja(Qur'an),Dini yetu ni
moja(uislaam).
Mtume(s.a.w) aliwaambia Waislaam "ENYI MLIOAMINI
MUOGOPENI MWENYEZI MUNGU UKWELI WA KUMUOGOPA,WALA MSIFE ISIPOKUWA NI
WAISLAAM.NA SHIKAMANENI PAMOJA KATIKA DINI YA MWENYEZI MUNGU NA WALA
MSIGAWANYIKE!NA KUMBUKENI NEEMA ZA MWENYEZI MUNGU JUU YENU,PINDI
MLIPOKUWA MAADUI BASI AKAZIUNGANISHA NYOYO ZENU NA MKAWA NDUGU KWA NEEMA
YAKE(QUR'AN).NA MLIKUWA KATIKA UKINGO WA SHIMO LA MOTO BASI AKAKUOKOENI
NALO.NAMNA HIVYO MWENYEZI MUNGU ANAKUBAINISHIENI AYA ZAKE ILI MPATE
KUONGOKA!"(Qur'an 3:102-103)
Kwa hiyo Mtume alikuwa akilingania
Umoja baina ya Waislaam wenye utaratibu mmoja,ambapo Mwenyezi Mungu
alimtaka Mtume awakumbushe Historia yao waliokuwa Waislaam kuwa wamekuwa
wamoja,ndugu badala ya hali ya utengano na uadui waliokuwa nao kabla ya
kuwa Waislaam.Kwahiyo Uislaam ulikuwa ni mmoja,kundi moja-Kundi la
Mwenyezi Mungu(Qur'an 58:22) na ni marufuku kuanzisha kundi ndani ya
kundi moja la Uislaam!Bali kulikuwa na kundi lingine ambalo ni kundi la
Shetani ambalo lilikuwa ni dhidi ya Waislaam.
Mara fulani kule
Madina Wanafiki walijaribu kuanzisha Msikiti na wakamuomba Mtume aende
kuuzindua.Mtume(s.a.w) kwa kuwa hakuwa akijua Ghaibu(Siri)
aliwakubalia,lakini Allah mjuzi wa Ghaibu alimkataza Mtume wake asiende
kuuzindua Msikiti huo kwa kuwa waanzilishi wake hawakuwa na lengo zuri
katika kuuanzisha Msikiti huo "NA WALE WALIOTENGENEZA MSIKITI KWA AJILI
YA KULETA MADHARA NA UPINZANI NA KUWAGAWA WAUMINI,NA KUWA SEHEMU YA
KUJIFICHIA YA WALE WALIOMPIGA VITA MWENYEZI MUNGU NA MTUME WAKE
ZAMANI......"(Qur'an 9:107).
Ndio kusema kuwa hao walikuwa ni
wanafiki ambao Mwenyezi Mungu aliwaumbua!Kumbe miongoni mwa malengo yao
ni kuwagawa Waumini!wasiwe kitu kimoja kwa manufaa yao binafsi kinyume
na agizo la Mwenyezi Mungu la kuwataka Waislaam wawe ni kitu
kimoja,kundi moja lisilo na mpasuko wala mgawanyiko!Mtume akaambiwa
"USISIMAME KAMWE NDANI YA MSIKITI HUO..."(9:108)
Ndugu zangu njama
za kuwagawa Waislaam zilendelea na kufanyiwa juhudi kubwa tangu enzi za
Uhai wa Bwana Mtume Muhammad(s.a.w).Mtume aliwaasa Waislaam kwa
kuwaambia hali akiwaonya "WALA MSIWE KAMA WALE WALIOGAWANYIKA NA
KUTOFAUTIANA,BAADA YA KUFIKIWA NA UBAINIFU.NA HAO NDIO WATAKAOPATA
ADHABU KUBWA KABISA"(Qur'an 3:105).Kumbe tulishonywa kuwa "Wala tusiwe
kama wale!"Ina maana walikuwepo watu walikuwa wameigawa Dini yao na
wakatofautiana ndani yake!NI KINA NANI HAO?
Hao si wengine bali ni
wale waliopewa Uislaam zamani kisha wakauharibu kwa kuugawa makundi
makundi na kila kundi likawa linajiona liko sawa.Wana wa Israel walipewa
Uislaam kwenye Taurati kupitia Nabii Musa(a.s),wakaugawa Uislaam wao na
ukawa Uyahudi,ambao nao uligawika katika makundi(Madhehebu) ya
Uzayuni,Uothordox,Usquirs n.k.
Baadae wakapewa Injili kupitia Nabii
Isa(a.s),wakauharibu Uislaam wao na waukaufanya kuwa ni Ukristo,ambao
nao uligawika katika makundi(Madhehebu) ya Roman
Catholic,Lutheran,Anglican n.k.
Sasa Waislaam walitakiwa wasiwe kama
hao,wakati huo wao walikuwa ni kundi moja!wakaonywa tena "NYENYEKEENI
KWAKE NA MUMUOGOPE NA SIMAMISHENI SWALA,WALA MSIWE MIONGONI MWA
WASHIRIKINA.AMBAO WAMEIGAWA DINI YAO NA WAKAWA MAKUNDI MAKUNDI,KILA
KUNDI LINAFURAHIA WALIYONAYO"(30:31-32).
Tunapata hitimisho kuwa
kumbe Uyahudi na Ukristo ni Ushirikina kwa kuigawa Dini Makundi
Makundi(Madhehebu).Tena Allah akaonya kwa mara nyingine kuwa "NA
HAWATOKUWA RADHI NAWE MAYAHUDI NA WAKRISTO MPAKA UFUATE MILA YAO.SEMA
HAKIKA MUONGOZO WA MWENYEZI MUNGU NDIO MUONGOZO HASWA,NA KAMA UTAFUATA
MATAMANIO YAO BAADA ELIMU ILIYOKUFIKIA,HUTAPATA KUTOKA KWA MWENYEZI
MUNGU MLINZI WALA MSAIDIZI"(2:120).
Msiba ulioje Waislaam wamefuata
yale waliyokatazwa!Baada ya miaka kadhaa kupita tangu Mtume
kufariki,Waislaam wakagawika Makundi Makundi(Madhehebu)!Mpaka leo hii
Waislaam waliopewa Uislaam katika Qur'an kupitia Mtume Muhammad(s.a.w)
wameugawa Uislaam wao na umekuwa ni Usunni,Ushia,Uanswaar
Sunna,Uahmadiyya n.k. na katika hayo makundi kuna makundi mengine madogo
madogo ndani yake!
Sasa kuhusiana na mambo kama hayo Mtume
aliambiwa na mapema kwamba "HAKIKA WALE WALIYOIGAWA DINI YAO NA WAKAWA
MAKUNDI MAKUNDI HUNA UHUSIANO NAO WOWOTE,BILA SHAKA JAMBO LAO HILO LIPO
KWA MWENYEZI MUNGU,KISHA ATAWAAMBIA YALE WALIYOKUWA WAKIYATENDA"(6:159).
SOMO LITAENDELEA.....
Lakini kwa sasa,Hebu tujadili kwa pamoja,Ni kitu gani
kilichowasababisha Waislaam kuwa na Makundi wakati muongozo wao umekemea
waziwazi tena kwa maonyo makali ya Ushirikina na Ukafiri?.Na
je,Waislaam wanaweza kurudi katika Uislaam mmoja kama alouacha
Mtume(s.a.w)?
No comments:
Post a Comment